BAADA YA KUTUHUMIWA KUGAWA URODA KWA DIAMOND, IRENE UWOYA AMEFUNGUKA NA KUTOA KAULI MOJA NZITO SOMA HAPA




Baada ya habari nyingi kuhusu Irene Uwoya kufumaniwa na Diamond kutawala vyombo vya habari mitandao hapo juzi, bongomovies  iliamua kumtafuta kwa simu  Irene Uwoya ili kuweza  kupata  majibu  ya tuhuma   za yeye kuingilia penzi lwa mwanadada Penny....

Bongomovie  inadai  kuwa ,jana tangu asubuhi  ilikuwa  ikimtafuta  Irene  Uwoya  hewani  bila  mafanikio  kwa  kuwa  simu  yake  ilikuwa  ikiita  bila  kupokelewa....

Saa kumi na mbili hivi jioni, bongomovie hatimaye  ilifanikiwa kumpata Uwoya  hewani na  kumtwisha  zigo  hilo  la  lawama  na  maswali  kibao  kuhusu  kufumaniwa  na  Diamond.....

Bongomovie  inadai  kuwa, Uwoya  alishindwa  kujibu  tuhuma  hizo  na  kutoa  jibu  moja  na  fupi  la  mkatona .."ACHANA  NAZO, HAZIWAHUSU"

Kundi  zima  la bongo movie  likaona  isiwe tabu ....likaamua  kumwacha  binti  huyo  .Hata  hivyo kwa  mtu  yeyote  mwenye  umakini wa  kufikiri  atakuwa  amekwisha elewa Uwoya  alimaanisha  nini...!!

Comments