PAIN KILLER" NI FILAMU MPYA YA HEMED "PHD" ILIYOINGIA SOKONI



Mwanamuziki na muigizaji filamu Hemed Phd, ambaye wakati huu video yake ya’Going Crazy’ bado inafanya poa, ameamua kuachia rasmi filamu yake mpya ambayo inakwenda kwa jina ‘Painkillers’.

Filamu hii tayari imekwishaanza kupokelewa vizuri mitaani jambo ambalo tayari linaashiria kuwa mauzo yake yanaweza kufikisha rekodi nzuri ndani ya kipindi kifupi tu tangu kuachiwa kwake.

Filamu hii mpya ni ishara nyingine pia kwa Mashabiki wa Hemed kuwa yeye ni msanii wa ukweli kutokana na kuwa na kipaji zaidi ya kimoja, na anamudu vizuri kuvitumia vyote kwa ajili ya kuwapa watu burudani ile wanayopenda

Comments