Seikali ya Nepal yasema inasimamia vyema utoaji wa misaada kutokana na tetemeo kubwa la ardhi lililowakumba





 
 wanajeshi wakitoa misaada Nepal.

Serikali ya Nepal imejitetea dhidi ya lalama kwamba inashindwa kusimamia vyema misaada ya dharura, kufuatia tetemeko kubwa la ardhi hapo Jumamosi.


Mkuu wa masuala ya dharura wa Nepal Rameshwor Dangal,ameambia BBC serikali inajitahidi iwezavyo, lakini mkasa huo ulikumba majimbo 20 nchini, na hivyo mahitaji ni mengi sana ndiposa serikali inalemewa.

Hali ya kutamauka imewakumba wengi waliothiriwa na tetemeko hilo,na wengine wameonesha malalamiko yao kwa kulumbana na polisi huko Kathmandu, mji mkuu wa taifa hilo.Maelfu wameanza kuuhama mji huo mkuu.


Angalau sasa misaada ya bidhaa muhimu na huduma zimeanza kuwafikia mwaavijiji.
Wakati huo huo, Mwanamme aliyetolewa ndani ya vivusi katika hoteli iliyoporomoka mjini Kathmandu ameelezea jinsi aliweza kuishi kwa saa 82 kabla ya kuokolewa.
Rishi Khanal amesema alilazimika kunywa mkojoo wake wakati akisubiri kuokolewa.

Mguu wake alikwamba ndani ya vivusi lakini aliweza kuwasiliana na jamaa zake akitumia simu yake ya mkononi.
Hata hivyo hakumbuki hoteli alimokua. Aliokoewa na makundi ya wokozi kutoka Nepal na Ufaransa.

Zaidi ya watu elfu 5 wameuawa katika janga hilo la maporomoko ya ardhi huko Nepal.

Comments