37 wanaswa kwa wizi wa maji Dar
Mitambo ya maji.
Kukamatwa
kwa watu hao kunafuatia operesheni inayofanywa na Kampuni ya Majisafi
na Majitaka (Dawasco) na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (Dawasa)
inayomiliki miundombinu ya huduma hiyo.
Mamlaka
hizo ziliamua kuendesha operesheni hiyo kufuatia kukithiri kwa wizi wa
maji na hivyo kuwasababishia wakazi wengi wa Jiji la la Dar es Salaam
kukosa huduma hiyo muhimu
.
Wizi
huo ni pamoja na ule wa kukwepesha mita, kujiunganishia, kukatisha
laini na kusababisha wakazi wa eneo husika kukosa maji huku yakiuzwa kwa
wafanyabiashara ambao nao huwauzia wananchi kwa bei kubwa.
Mmoja
wa wafanyakazi wa Dawasa, alisema wakazi wengi wa Magomeni, Vingunguti
walishangaa kuona mabomba yao yakitoa maji baada ya kukosa huduma hiyo
kwa takriban miaka mitatu.
Huduma hiyo ilirudishwa katika eneo hilo baada ya Dawasa kugundua wizi huo na kuunganisha upya.

Comments
Post a Comment