KESI MAANDAMANO YA WAISLAMU:Shahidi: Nilikamatwa nikitoka msikitini

Wakili wa Utetezi, Mohammed Tibanyendera
Shahidi  wa utetezi katika kesi inayowakabili watu 54 ya kufanya maandamano isivyo halali, ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwamba alikuwa ana taarifa ya kuwapo kwa maandamano ya Waislamu kwa sababu alihudhuria mkutano wa hadhara na pia alisikia kwenye vyombo vya habari
.
 
Shahidi huyo wa 31 wa upande wa utetezi, Bakari Athumani, alidai kwamba siku ya tukio, alikuwa anatoka msikitini kuelekea Kidongo Chekundu, lakini alipofika mtaa wa Uhuru na Mnazi Mmoja, alikamatwa na polisi bila kujua kosa lake.
 
“Nilikuwapo kwenye kongamano la Kiislamu lililofanyika  mwishoni mwa Februari Temeke ambapo Shekh Juma Bungo, aliwasisitiza Waislamu wote kuandamana Februari 15, mwaka huu endapo Sheikh Ponda Issa Ponda, hatapewa dhamana. Lakini mimi binafsi sikuandamana kwa sababu sipendi kufanya hivyo,’’ alisema Athumani.
 
Alitoa ushahidi huo mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Sundi Fimbo.
 
Washitakiwa wengine wa upande huo wa utetezi walidai kwa nyakati tofauti kuwa hawamfahamu Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) cheo chake wala hawajui ofisi yake ilipo.
 
Wakili wa Utetezi, Mohammed Tibanyendera, aliyewaongoza washtakiwa.
 
Washtakiwa hao kwa nyakati tofauti walidai kuwa hawamfahamu Sheikh Ponda wala hawafahamu kesi yoyote kuhusiana na Masheikh inayoendelea mahakamani hapo. 
 
Ushahidi wa upaande wa utetezi katika kesi hiyo utaendelea kusikilizwa leo.
 

Comments

Popular Posts