Kesi ya kina Ponda yaibua mapya
Sheikh Ponda Issa Ponda
Shahidi huyo alitoa madai hayo jana alipokuwa anatoa utetezi wake mbele ya Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Victoria Nongwa.
Salma alidai kuwa askari hao walivunja mlango mkubwa na kuingia
msikitini na kuwakuta wanaume wanaswali, mmoja akasema ndani kuna watu
wengine ambao walikuwa wanawake wakaamriwa kutoka.
Alidai watu hao walijitambulisha kuwa ni askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) wakawaamuru kunyoosha mikono juu.
‘’Walitutukana matusi pamoja na kutukebehi, nikawaomba kwenda
kuchukua pochi yangu niliyokuwa nimeisahau ndani ambayo iliyokuwa na
Shilingi 780,000 wakaniambia hakuna ruhusa,” alidai.
Naye shahidi wa 22, Said Rashid alidai kuwa siku ya tukio alikuwa
kwenye Msikiti uliopo kiwanja cha Marcus Chang’ombe na hatambui shtaka
linalomkabili wala halifahamu Baraza la Waislamu Tanzania (Bakwata).
Mashahidi kumi walitoa utetezi wao mahakamani hapo na kufanya jumla ya washahidi waliotoa ushahidi kufika 27.
Ushahidi unaendelea leo.
Upande wa wa mashtaka ulidai kuwa katika shtaka la kwanza, Oktoba
12, mwaka huu huko Temeke jijini Dar es Salaam, washtakiwa wote 50
walikula njama ya kutenda makosa.
Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa siku ya tukio la kwanza katika
eneo la Chang’ombe Markas, Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam,
washtakiwa wote 50 kwa jinai walivamia kwa nia ya kutaka kujimilikisha
kiwanja mali ya Agritanza Ltd.
Katika shtaka la pili, Ilidaiwa kuwa kati ya Oktoba 12 na 16, mwaka
jana eneo la Chang’ombe Markas pasipo uhalali na hali ya uvunjifu wa
amani washtakiwa wote kwa pamoja walijimilikisha ardhi ambayo ni mali ya
Agritanza Ltd.
Shtaka la nne, ilidaiwa kuwa kati ya Oktoba 12 na 16, mwaka jana
katika eneo hilo, washtakiwa waliiba vifaa mbalimbali vya ujenzi ikiwemo
matofali 1,500, tani 36 za kokoto na nondo vyote vikiwa na thamani ya
Sh. 59,650,000 mali ya Agritanza Ltd. Wote walikana mashitaka hayo.

Comments
Post a Comment