Mawakala Redd's Miss TZ kunolewa leo
Mkurugenzi na mratibu wa shindano hilo kutoka katika kampuni ya Lino International Agency, Hashim Lundenga
Akizungumza na JAMIILEOTZ jana, mkurugenzi na mratibu wa shindano
hilo kutoka katika kampuni ya Lino International Agency, Hashim
Lundenga, alisema kuwa mawakala watakaoshiriki semina hiyo ni wa kuanzia
ngazi ya kanda, mikoa na vitongoji vyote vya mkoa wa Dar es Salaam.
Lundenga alisema kuwa maandalizi ya semina hiyo yamekamilika na
mawakala kutoka mikoani walianza kuwasili jijini tangu jana asubuhi na
katika mialiko waliyotumiwa wamesisitizwa kufika bila kukosa ili kupata
maelekezo kabla ya kuanza kuandaa mashindano yao ya ngazi husika.
Alisema kuwa kila mwaka kamati yake hutoa maelekezo kulingana na
kanuni na taratibu zilizopitishwa na kamati hiyo na vilevile kuwapa
mwangaza mawakala ni makampuni na taasisi zipi wanazoruhusiwa kuomba
udhamini ili wasiende tofauti na mdhamini mkuu wa shindano hilo ngazi ya
taifa.
"Tunaamini semina itafanyika kama ilivyokusudiwa na mawakala
watapewa mbinu za kukabiliana na changamoto mbalimbali katika kutekeleza
majukumu yao," alisema Lundenga.
Mrembo kutoka katika kitongoji cha Sinza, kanda ya Kinondoni jijini
Dar es Salaam, Brigitte Alfred, ndiye anayeshikilia taji hilo la taifa
aliyelitwaa kutoka kwa Salha Israel wa Ilala.
Mwaka jana, kalenda ya mashindano hayo ilibadilika ambapo Kamati ya
Miss Tanzania ilieleza kuwa mshindi Brigitte ataiwakilisha nchi katika
mashindano ya dunia mwaka huu na mrembo atakayeshinda taji hilo baadaye
mwaka huu ndiye atakayeshiriki fainali hizo mwakani.
Lundenga alisema kuwa lengo la mabadiliko hayo ni kumpa mshindi
nafasi ya kujiandaa vyema kushiriki fainali hizo zinazoshirikisha
warembo kutoka nchi zaidi ya 100.
Rekodi ya mrembo wa mwaka 2005, Nancy Sumary, aliyetwaa taji la
Mrembo wa Dunia Kanda ya Afrika haijavunjwa na washiriki wengine
waliowahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo

Comments
Post a Comment