Mbunge Chadema kizimbani
Mbunge wa jimbo la Ukerewe, Mwanza kwa tiketi ya Chadema, Salvatory Machemli
Machemli (39) amesomewa shitaka hilo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya wilaya hiyo, Rouben Luhasha.
Hata hivyo, Machemli amekana shitaka hilo na yupo nje kwa dhamana ya Sh. milioni 2 na ahadi ya Sh. 150,000.
Mwendesha mashitaka wa polisi ASP, Denis Rwiza, alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Oktoba 23, 2011 majira ya saa za alasili katika kijiji cha Nyamanga kisiwani Ukara.
Rwiza ambaye pia ni Afisa Upepelezi wa wilaya hiyo, alisema mbunge huyo alitenda kosa hilo wakati akihutubia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Chadema.
Alisema mshitakiwa kwa makusudi aliwachochea wananchi kutenda kosa hilo kwa kuwaelekeza wachukue uamuzi mgumu ikiwa ni pamoja na kuzuia na kushambulia maafisa wa polisi wakati wa kufanya kazi zao kisiwani hapo.
Imedaiwa kuwa kupitia mkutano huo aliwataka wananchi wazuie na wamshambulie kwa silaha za jadi ikiwemo marungu, mapanga na fimbo afisa wa polisi atakayekwenda kutafuta washitakiwa nyakati za usiku.
Mwendesha mashitaka huyo wa polisi alisema kipindi hicho ulikuwepo msako wa watuhumiwa wa mauaji ya watu wanne waliouawa na wananchi Desemba 10, 2010 mbele ya maafisa wa polisi kwa tuhuma za ujambazi.
Upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na imeahailishwa hadi Machi 21, itakapotajwa tena

Comments
Post a Comment