MWAKYEMBE.......UFISADI MPYA BANDARINI
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe
Madai hayo yameibuka baada ya kila wanapotaka kupitisha mizigo yao kulazimishwa kutoa rushwa.
Walimweleza hayo juzi Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe,
wakati wa mkutano wa dharura wa wakurugenzi wa makampuni ya mawakala wa
Forodha kueleza changamoto zinazowakabili katika Bandari ya Dar es
Salaam.
Mmoja wa mawakala hao, Teddy Mwakibete, alisema katika kero
wanazokumbana nazo katika bandari hiyo ni pamoja na kuombwa rushwa
wanapotaka kupitisha mizigo ambayo imekamilishwa taratibu zote za
kisheria.
“Geti zote zilizowekwa bandari zimewekwa kwa ajili ya kunufaisha
baadhi ya watu hasa geti la kuingilia Kampuni ya Kupakua na Kupakia
Makontena (TICS), tunalazimishwa kutoa rushwa ndipo tupite,” alisema
Mwakibete.
Mwakibete alimweleza Dk. Mwakembe kero nyingine wanayokumbana nayo
mawakala wa forodha ni kulazimishwa kuwa na rundo la vitambulisho ili
waruhusiwe kufanya kazi zao vinavyowagharimu zaidi ya Sh. 64,000.
Mfano wa vitambulisho hivyo ni cha TICS, TPA (Mamlaka ya Bandari),
ICD na cha uwanja wa ndege ambavyo vinawagharimu pesa nyingi na hutakiwa
kuvivaa kwa wakati mmoja.
Wakala mwingine, Otieno Igogo, alisema serikali isadie kuweka
ushindani mzuri wa kibiashara kwa mawakala kwa sababu mawakala wakubwa
wanawaonea wadogo na kuwachongea kwamba ni wezi na matapeli.
Igogo alisema kero nyingine inayowakabili ni upatikanaji wa leseni
ya wakala wa forodha ambayo ni ngumu kuipata kutokana na sheria
zilizowekwa.
"Mheshimiwa waziri kuna tatizo la makampuni makubwa kukusanya fedha
ambazo ni za tozo na kuzipeleka nje, hili suala lazima serikali
iliangalie linaathiri uchumi wan nchi,” alisema Igogo.
Akijibu malalamiko hayo, Dk. Mwakyembe alisema suala la mawakala
kutakiwa kuwa na vitambulisho vingi atalifanyia kazi kwa kuhakikisha
kunakuwa na kitambulisho kimoja tu au viwili.

Comments
Post a Comment