Polisi yazuia maandamano ya kudai maji Dar
Kamanda wa Polisi mkoa wa kinondoni, Charles Kenyela
Kamanda wa Polisi mkoa huo, Charles Kenyela, alisema maandamano
hayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa amani pamoja na kuhatarisha
usalama wa raia na mali zao.
Alisema maazimio hayo yametolewa baada ya kupokea barua mbili
kutoka kwa Mnyika mapema wiki hii na kukusanya na kubadilishana taarifa
na wadau mbalimbali ambao wangeguswa na mkutano pamoja na maandamano
hayo.
Kenyela alisema walibaini kuwa taarifa ya hoja hiyo tayari Mnyika
amekwishaiwasilisha katika Bunge, hivyo Waziri mwenye dhamana alitakiwa
kuijibu hoja hiyo katika Bunge na hivyo siyo utaraibu mzuri kwani
unaonyesha kuashiria kuchochea fujo kwa kuwa majibu ya suala hilo anayo
kupitia Bunge.
Sababu nyingine kuwa ni kuwa eneo la Manzese Bkharesa ambalo
limekusudiwa kufanyika mkutano huo ni la kuegeshea magari na liko kando
ya barabara ambayo kwa sasa iko katika ujenzi hivyo si mahali sahihi pa
kufanyia mikutano.
Kamanda Kenyela alisema pia Waziri husika ambaye maandamano
yanakwenda katika ofisi zake hana taarifa yeyote juu ya maandamano hayo
na kwamba kwenda kwa maandamano katika ofisi za serikali bila kutoa
taarifa rasmi ni sawa sawa na kuwachochea wananchi dhidi taasisi yao ya
Serikali jambo ambalo amesema linaweza kusababisha fujo na kutokea kwa
vurugu.
Aliitaja sababu nyingine kuwa ni ufinyu wa barabara ya Morogoro ambayo maandamano yanatakiwa kufanyikia.
Aliongeza kuwa eneo la Wizara ya maji ni eneo finyu na limepakana
na kituo cha Gridi ya Taifa ya umeme, gesi ya Ubungo na lipo karibu na
kituo cha daladala, maeneo ambayo yana watu wengi na wanaweza kudhurika
endapo fujo zitatokea.
“Jeshi la Polisi limeyabaini hayo ambayo nimeyaeleza na kuamua
kuzuia kufanyika kwa maandamano hayo, hivyo yeyote atakayekaidi agizo
hili hatua kali za kisheria zitachukuliwa,” alisema Kenyela. Hata hivyo,
Mnyika jana hakupatikana kuzungumzia hatua hiyo.

Comments
Post a Comment