HABARI YA PINDA KUWASHA MOTO KWENYE MACHIMBO YA MORAMU ARUSHA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akiweka saini katika kitabu cha maombeleo mbele ya majeneza ya watu waliofariki dunia kwenye machimbo ya moramu eneo la Moshono mkoani Arusha juzi. Waziri Mkuu alikwenda kuwapa pole ndugu wa marehemu hao jana
Waziri Mkuu Mizengo Pinda, amesema machimbo ya moramu yaliopo Moshono nje kidogo ya jiji la Arusha, yatafungwa kwa muda tu na kufunguliwa, baada ya serikali kuhakikisha usalama wa eneo hilo, ili liendelee kutoa ajira kwa vijana.
Waziri Mkuu Pinda wakati alipokuwa akitoa salamu za pole kwenye uwanja wa kuhifadhi maiti Hospitali ya Mkoa Mount Meru, ambako majeneza 13 yalikuwa zimeshaandaliwa tayari kwa mazishi na baadaye kutembelea eneo la machimbo.
 
Alisema mchimbo hayo yaliyosababisha vifo vya watu 13 na majeruhi wawili, yamesitishwa kwa muda, ili wataalam kuangalia uwezekano wa kutathimini eneo hilo na kisha yatafunguliwa, ili yaendelee kutoa ajira kwa vijana.
 
“Hatuwezi kuyafunga moja kwa moja sababu haya yanategemewa sana na wakazi wa Arusha na pia ni eneo moja muhimu kwa ajira kwa vijana wetu, muhimu kuweka mazingira salama,” alisema.
 
Aidha, alipongeza uongozi wa jiji, viongozi wa vyama vya siasa na dini, kwa kuweza kuhakikisha miili ya marehemu inasitiriwa vizuri na kuzikwa kwa taratibu zote.
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, alisema watu 15 ndio waliopata maafa hayo, lakini kati yao 13 walifariki baada ya na mmoja aitwaye Maliek Lenanu (40) amelazwa hospitali ya Mount Meru baada ya kuangukiwa na jiwe kifuani na kufunikwa na mchanga hadi juu ya kifua.
 
Majeruhi huyo amweleza Waziri Mkuu Pinda, kwamba anamshukuru Mungu kwa kuokolewa.
Naye Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema aliwapongeza viongozi wa jiji la Arusha kwa kujitahidi kuokoa roho za marehemu hao, lakini ilishindikana kuokoa uhai na kufanikiwa kupata miili yao.
 
Marehemu hao ni Japheti Neilyang, Gerald Neilyang, Japhet Raphael, Elibariki Loserian, Fabian Bambo, Fred Loserian, Elias Fanuel, Wilbrart Raphael, Christopher Kawishe, Gerald Masai, Julus Pallangyo, Gerald Jacob na Alex Maliaki.
 
Majeruhi mmoja ambaye hakutajwa jina alitibiwa juzi na kuruhusiwa kwenda nyumbani.
Simanzi na vilio vilitawala hospitalini hapo baada ya majeneza hayo kuwekwa nje ya chumba cha kuhifadhia maiti na kisha kuombewa na viongozi mbalimbali waliohudhuria sala hiyo na  wanandugu kuchukua miili ya kila mmoja na kwenda kuzika.
 
Ibada hiyo ilihudhuriwa na wabunge wa Mkoa wa Arusha, viongozi wa dini pamoja na wafuasi wa vyama mbalimbali.
 
Wakati huo huo, Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Arusha na kuwapa pole wafiwa pamoja na majeruhi

Comments

Popular Posts