MAAJABU WATOTO 54 WAZALIWA KWENYE SKUKUU YA PASAKA MOROGORO

Baadhi ya wakinamama waliojifungua siku ya Pasaka wakiwa na watoto wao.
Watoto 54 wamezaliwa katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro katika kipindi cha sikuu ya Pasaka.
 
Kati ya watoto hao waliozaliwa kuanzia  Ijumaa Kuu, siku ya kuteswa kwa Yesu Kristo na kufufuka kwake Jumapili ya Pasaka wa kike ni 28 na kiume   26.
 
Akizungumza kwa niaba ya Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Muuguzi Mkuu wa zamu,Yohana Sehaba alisema kuwa watoto hao ambao walizaliwa baada ya mama zao kufikishwa hospitalini hapo wakati wa mkesha wa Ijumaa Kuu na wa Pasaka, hali zao zinaendelea vizuri.
 
“ Watoto wote waliozaliwa wakati wa Ijumaa Kuu hadi leo jumatatu tunavyo sherehekea Pasaka wote wazima na afya zao njema  baadhi yao wameruhusiwa na wengine bado wanaendelea na matibabu madogo,” alisema Sehaba.
 
Alisema kati ya watoto hao  tisa walizaliwa kwa njia ya upasuaji na hali za mama zao hali zao zinaendelea vizuri.
 
Kwa upande wake, Muuguzi Mkunga wa zamu, Happy Matovu, alisema  hakuna matatizo yoyote waliyopata watoto hao  wakati mama zao  wakijifungua.

Comments

Popular Posts